• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

AFISA ELIMU MKOA WA MBEYA ATOA NASAA KWA WALIMU CHUNYA.

Imewekwa: January 16th, 2026

Afisa elimu Mkoa wa Mbeya Mwl. Farida Mwasumilwe ametoa nasaa mbalimbali kwa walimu wa Shule za Msingi ili kuendelea kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi ikiwa ni pamoja na taratibu za usajili wa wanafunzi, uzaji wa taarifa mbalimbali kwenye mfumo wa ukusanyaji taarifa Shuleni, utawala bora, uwajibikaji , usimamizi wa rasilimali na miradi ya shule pamoja na mambo mengine mengi.

Nasaa hizo amezitoa leo tarahe 16/01/2026 wakati wa kikao cha tathimini na kuweka malengo au matarajio ya taaluma kwa mwaka 2026 na walimu wa taaluma, walimu wakuu na maafisa elimu shule za msingi kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Sapanjo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Niwaombe tuzingatie muda wa usajili kulingana na taratibu za baraza la mitihani, lakini pia kwa shule binafsi kulipa malipo ya mitihani ya watahiniwa  kwa wakati , lakini suala jingine niombe tutumie kikamilifu mfumo wa ujazaji taarifa Shuleni (SIS) ikiwa ni pamoja na masuala ya likizo,maudhurio ya wanafunzi na mambo mengine mbalimbali”.amesema Mwl Farida.

Aidha, Mwl Farida ameendelea kuwakumbusha Shule binafsi kuhakikisha zinaendelea kuzingatia taratibu na miongozo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikataba ya ajira kwa watumishi wao na kuwachangia katika mifuko mbalimbali, kuzingatia taratibu za usajili wa wanafunzi hususani wanaohamia  na mambo mengine mengi.

Vilevile, Mwl Farida amesisitiza suala la utawala bora ikiwa ni pamoja na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu mbalimbali, kuwa wazi katika taarifa za fedha ,kuzingatia taratibu na miongozo mbalimbali ya shule pamoja na uzimamizi bora wa rasilimali za Shule ikiwemo thamani mbalimbali za Shule na miundombini.

Wakizungumza kwa niaba ya walimu wengine walioshiriki kikao hicho Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Kiwanja, Mwl. Hadija Issa amesema wamejipanga kuhakikisha Wilaya ya Chunya inaongoza kwenye ufaulu wa matokeo ya darasa la nne na darasa la saba kwa mkoa wa Mbeya.

“Tumejipanga kimatokeo kuongeza ufaulu zaidi, kwa changamoto zilizojitokeza kwenye matokeo ya mwaka 2025 tunazifanyia kazi na kuongeza ufaulu kwa mwaka huu 2026, tunataka kuwa namba moja kwa mkoa wa Mbeya kwenye matokeo ya darasa la nne na darasa la saba” amesema Mwl. Hadija.

Kwa upande wake Mwalimu Frank Sanga wa Shule ya Msingi Mapongolo, amesema, sasa ni wakati wa kuyafanyia kazi mapungufu yote tuliyoyabaini kwenye tathmini ya kikao hicho ambapo kwa mwaka huu 2026 hawatarudi nyuma tena, wamejipanga kupandisha kiwango cha taaluma kwa shule za msingi Wilaya ya Chunya.

 Kikao hicho mbali na kutoa nasaha pia  kimesikiliza kero mbalimbali za walimu, changamoto, na kuangazia njia za utatuzi wa changamoto hizo kwa lengo la la kuboresha ili kujipanga  kufanya vizuri kitaaluma na kuifanya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuwa mfano wa kuigwa kitaaluma na Halmashauri nyengine Mkoa wa Mbeya.

Washiriki wa kikao cha tathmini na malengo ya taaluma kwa mwaka 2026 Wilaya ya Chunya wakifuatilia kwa makini hotuba ya Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya Mwl. Farida Mwasumilwe. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Sapanjo leo tarehe Januari 16, 2026.

Afisa elimu Mkoa wa Mbeya Mwl. Farida Mwasumilwe akitoa hotuba yake kwa washiriki wa kikao cha tathmini na malengo ya taaluma kwa mwaka 2026 Wilaya ya Chunya. Kikao kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Sapanjo leo tarehe Januari 16, 2026.

Washiriki wa kikao cha tathmini na malengo ya taaluma kwa mwaka 2026 Wilaya ya Chunya wakifuatilia kwa makini hotuba ya Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya Mwl. Farida Mwasumilwe. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Sapanjo leo tarehe Januari 16, 2026.

Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • AFISA ELIMU MKOA WA MBEYA ATOA NASAA KWA WALIMU CHUNYA.

    January 16, 2026
  • AFISA ELIMU MKOA WA MBEYA ATOA NASAA KWA WALIMU CHUNYA.

    January 16, 2026
  • KAMATI ZA UJENZI ZATAMBULIWA CHUNYA: MWENYEKITI ATUMA OMBI POLISI

    January 15, 2026
  • MKAWE MABALOZI WA MFUMO WA SIS KWA WALIMU WENGINE.

    January 14, 2026
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.