• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Tumieni mikopo ya ujasiriamali kwa manufaa-Mwanginde

Imewekwa: July 16th, 2022

WANUFAIKA wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wametakiwa kutumia mikopo hiyo kwa makini ili iwaletee manufaa.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Mh. Bosco Mwanginde wakati wa ziara ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ilipotembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri.

Mwanginde amewasisitiza wanufaika kuhakikisha mikopo wanayoipata wanaitumia kwa manufaa yao wenyewe na kujikwamua kiuchumi huku akiwataka wale wote ambao wamepatiwa mikopo kuhakikisha wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati ili watu wengine waweze kukopa.

Vile vile Mwanginde amesema kuwa kuna dhana potofu iliyojengeka miongoni mwa jamii kuwa mikopo hiyo ni hisani kwamba haitakiwi kujereshwa, hivyo kuwataka wanufaika hao kuondokana na dhana hiyo na kuhakikisha wanarejesha tena kwa wakati ili kila mtu mwenye sifa anayehitaji mkopo huo aweze kupatiwa.

“Lengo la mikopo hii ni kuhakikisha wananchi wote wenye sifa ya kupata mikopo wanapata kwa lengo la kuwainua kiuchumi, ndio maana nasisitiza kuirejesha tena kwa wakati kwani hii mikopo sio hisani kama baadhi ya watu wanavyodhani” Alisisitiza Mh Mwanginde.

“Sisi tunajua tayari tumewapa pa kuanzia kinachotakiwa ni kuendelea kutafuta faida ili sasa msiendelee tena kuitegemea Serikali.” Aliongeza Mwanginde.

Pia Mwanginde alitumia fursa hiyo kukipongeza kikundi cha HAPA KAZI TU kwa mwenendo mzuri wanaokwenda nao na kurejesha mkopo waliopatiwa kwa muda muafaka.

“Maeneo mengi tunakopesha fedha na hazirudi lakini kwa taarifa ya Afisa Maendeleo ya Jamii, ninyi mnakwenda vizuri hongereni sana,” alisema Mh Mwanginde.

Kwa upande wa miradi mingine iliyotembelewa na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Wajumbe wa Kamati wametoa pongezi kwa uongozi wa Halmashauri kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ubora na ufanisi mkubwa

Aidha wajumbe wameutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Miradi iliyotembelewa na kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ni pamoja na Vituo vya Afya Mafyeko, Kambikatoto na Sangambi, ujenzi wa nyumba ya watumishi 3/1 katika kituo cha afya Kambikatito, ujenzi wa majengo mbalimbali katika hospitali ya Wilaya

Kwa upande wa elimu kamati imetembelea mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari Lualaje sambamba na Shule ya Sekondari Mayeka.

Aidha kamati imetembelea ukamilishaji wa ujenzi wa soko la madini pamoja na jengo la utawala

Wajumbe wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya halmashauri ya wilaya ya Chunya walipotembelea vikundi vya vijana wa Bodaboda waliopatiwa mkopo wa asilimia 10 na Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Afisa Maendeleo ya Jamii Ndg Vincent Msolla akitoa maelezo kwa Waheshimiwa madiwani wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipanga ya Halmashauri walipotembelea na Kukagua kikundi cha Bodaboda kilichopatiwa mkopo wa Asilimia 10 toka Halmashauri

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.