• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TUKIONA MKAA INATOKA HUKU TUTAAMINI VIONGOZI WA SERIKALI MNAHUSIKA, MHE MANGINDE.

Imewekwa: April 6th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Said Mwanginde amewataka viongozi wote kushirikiana na wananchi kuhakikisha biashara ya Mkaa wilayani humo inakomeshwa haraka sana na amesema kuendelea kwa biashara hiyo ni ishara kwamba viongozi hao wanahusika na biashara hiyo hivyo hatua zitaanza kuchukuliwa dhidi yao

Ametoa kauli hiyo jana tarehe 5/4/2023 wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara Kitongoji cha Kambikatoto kilichopo kijiji cha Shoga kata ya Sangambi baada ya kuhitimisha zoezi la kutembelea na kuona uharibifu mkubwa wa Mazingira unaosababishwa na shughuli za Uchomaji wa Mkaa

“Sitaki mkaa utoke tena hapa kwa namna yoyote ile na kama tukiona mkaa unatoka huku basi sisi serikali tutaamini wajumbe wa serikali mnahusika hivyo tutaanza na ninyi viongozi na baadaye tuwafuate wale wale waharibifu wa mazingira. Haya ni amelekezo kutoka baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya”

Aidha Mhe. Mwanginde alimtaka mwenyekiti wa kijiji cha Shoga kuhakiki wananchi wanaoishi katika eneo hilo kama ni wakulima ili kuendana na mpango wa matumizi ya ardhi wa mwaka 2006 ambao unaonesha eneo hilo ni kwaajili ya kilimo na makazi hivyo shughuli zinazotakiwa eneo hilo ni kilimo sio uchomaji wa mkaa

“Mwenyekiti wa kijiji, anayetakiwa kuwepo hapa ni mkulima hivyo hakikini mashamba ya watu na asiye na shamba hatakiwi kuwepo hapa, anayetaka kukata mkaa afuate taratibu na kinyume na hapo basi tutamshughulikia ipasavyo” alisema Mwanginde

Awali akitoa salamu za kata kwa mwenyekiti wa halmashauri Diwani wa kata ya Sangambi Mhe. Junjulu Ndete amesema uharibifu wa mazingira ni mkubwa sana maeneo haya jambo ambalo halikubaliki kabisa, ameongeza kuwa kama hatutajipanga kulinda mazingira haya basi tutakaribisha ukame ambao utapelekea njaa kwetu sisi na taifa kwa ujumla.

“Miaka miwili iliyopita tulikuwa tunaenda Mnyolima, tulipotea njia tukapita hapa, Hali tuliyoikuta mwaka juzi tofauti kabisa na hali tuliyoiona leo, uharibifu wa mazingira ni Mkubwa mno” alisema Mhe Junjulu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya amehitimisha ziara iliyodumu kwa siku mbili tarehe 4/4/2023 na tarehe 5/4/2023 katika kata ya Sangambi ambapo lengo kubwa ni kukemea uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokana na shughuli za uchomaji mkaa katika kata hiyo na kupitia mikutano hiyo amewataka wananchi wote wilayani Chunya kushiriki zoezi la kutunza na kulinda Mazingira kwani ukame hauna mipaka.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde akizungumza na Wananchi juu ya umuhimu wa kutunza mazingira kwenye mkutano wa hadhara katika kitongoji cha Kambikatoto kilichopo kijiji cha shoga kata ya Sangambi

Mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde akishuhudia uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uchomaji wa Mkaa katika kijiji cha Shoga kata ya Sangambi

Diwani wa Kata ya Sangambi Mhe. Junjulu Ndete akieleza jambo kabla ya kumkaribishwa Mweshimiwa Mweyekiti wa halmashauri kuzungumza na wananchi wa kitongoji cha Kambikatoto 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.