• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SHULE YA SEKONDARI MASACHE KUANZA KUJENGWA ITUMBI.

Imewekwa: February 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe: Juma Zuberi Homera amesema azma ya serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha Mkoa wa Kimadini Chunya unatoka kwenye uzalishaji wa Dhahabu kilogramu 300 na kufika kilogramu 500 kwa mwezi na amewataka wachimbaji na wananchi kwa ujumla kuendelea kumunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali kwa ujumla ili lengo la kuwainua wananchi kiuchumi litimie

Amezungumza hayo jana (9/2/2023) akiwa katika siku ya pili ya ziara yake maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kimadini Chunya ambapo ametembelea wachimbaji wakubwa na wadogo Kijiji cha Itumbi, msitu wa Mbiwe, Makongolosi na Mwaoga ambapo amewataka kufanya kazi kwa bidii kwani serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa kila mtu kufanya shughuli za uchimbaji

Akiwa katika Kijiji cha Itumbi baada ya kusikiliza kero mbalimbali za wachimbaji na wananchi Mkuu wa Mkoa ameongoza Zoezi la Uchangishaji wa fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Shule ya sekondari ili kutatua kero ya kukosekana kwa sekondari eneo hilo, ambapo zaidi ya Milioni tatu zilipatikana, wananchi wakichangia Milioni moja laki tatu na ishirini na moja (1,321,000/=) na ofisi yake ikichangia milioni mbili (2,000,000/=)

Shule hiyo amependekeza kuitwa MASACHE SEKONDARI kama kumuuenzi Mbunge wa jimbo la Lupa, hata pindi atakapo maliza muhula wake, aidha kwa lengo la Mbunge huyo kuwa mlezi na Msimamizi tangu hatua za ujenzi mpaka kukamilika kwake

Aidha Mhe; Homera amewaonya viongozi wa serikali kuanzia ngazi za vijiji, kata na hata wilaya kutotumia vibaya nafasi zao kwa kuwanyanyasa wananchi jambo ambalo amesema sio lengo la serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Rais Mhe: Dkt Samia Suluhu Hassan.

“Watu wataendelea kuchimba madini na hakuna mtu atakaye wazuia, ninyi fuateni taratibu. Hata ninyi (wachimbaji wadogo) mnaweza kujiunga pamoja mkaenda ofisi za Madini na kwa wakala wa misitu (TFS) mkaomba kibali ili mpate maeneo ya uchimbaji kwenye msitu wa mbiwe na hakuna atakaye waondoa”

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amewataka wachimbaji hao wanapopata faida katika uchimbaji wa dhahabu kuhakikisha wanawekeza Chunya kwani muda utafika ambapo hawataweza kufanya kazi hiyo tena hivyo unahitaji kuwa na eneo la kuishi na hata kukuingizia kipato

“Mnapopata pesa angalau asilimia hamsini (50%) wekezeni kwa kujenga nyumba za biashara, hoteli na biashara nyingine kwaajili ya kupata pesa na maisha yako ya baadaye”

Muhifadhi misitu wilaya ya Chunya Ndugu. Innocent Lupembe akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa amesema msitu wa Mbiwe ni hifadhi ya serikali kuu na inahifadhiwa kwa lengo la kuhifadhi na kutunza vyanzo vya maji, hivyo tunawakaribisha wananchi na wawekezaji kuja kuomba kibali cha uchimbaji huku utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji unazingatiwa

“Haturuhusu miti kukatwa ndani ya hifadhi, miti yote inayotumika katika shughuli za uchimbaji ndani ya hifadhi hii (Mbiwe) inatoka nje ya hifadhi, tunawakaribisha wadau kuja kuomba vibali vya uchimbaji wa madini katika msitu wa Mbiwe”

Afisa madini Mkazi wa Mkoa wa kimadini Chunya Eng. Nyansiri Sabai amesema wachimbaji katika Mkoa wa Kimadini Chunya wanafuata sheria na taratibu zote za uchimbaji wa madini huku akiwakaribisha wadau wengine kuwekeza kwenye madini kwakufuata taratibu

“Watu hawa wanatekeleza sheria na wengine wanakaribishwa lakini wafuate utaratibu”

Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya imedumu kwa siku mbili katika mkoa wa kimadini chunya ambapo ametembelea maeneo mbalimbaji ya uchimbaji ili kujionea na kusikiliza kero za wachimbaji wakubwa na wadogo na kuzitatua zinazowekekana kwa wakati huo na kutafuta suluhu kwa zile ambazo hazikuwezekana kwa wakati huo

Wananchi wa Kijiji cha Itumbi wakiwa kwenye Mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera wakati wa ziara yake ya Kutembelea sekta ya madini katika Mkoa wa Kimadini Chunya

Muonekano wa kijiji cha Itumbi kata ya Matundasi wilayani Chunya.

Wachimbaji wadogo wadogo wa Dhahabu katika kijiji cha Itumbi wilayani Chunya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera wakati wa ziara yake ya kutembelea sekta ya madini katika mkoa wa kimadini Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.