• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SERIKALI KUPITIA OFISI YA RAIS TAMISEMI IMEJIPANGA KURUDISHA HADHI YA WALIMU CHUNYA

Imewekwa: May 31st, 2024

Mkurugenzi msaidizi Elimu anayesimamia elimu ya awali na Msingi Kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mwalimu Suzana Nussu amesema Serikali ya Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan imedhamilia kurudisha hadhi, heshima na thamani ya walimu nchini Tanzania Jambo ambalo litapelekea kufanya kazi kwa kujituma na kwa kujiamini wawapo katika kutekeleza majukumu yao na kwa kufanya hivyo itaongeza ubora wa Elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi wanapohitimu ngazi mbalimbali za Shule.

Ametoa kauli hiyo Leo tarehe 31/5/2024 wakati akizungumza kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) mbele ya walimu kutoka Idara ya elimu awali na msingi pamoja na walimu kutoka idara ya Elimu Sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake baada ya kuhitimisha ziara kama hiyo Mkoa wa Songwe.

“Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) tunataka hadhi, heshima na haki ya Mwalimu irudi. Hatuwezi kutekeleza hayo kwa kukaa ofisini hivyo ofisi nzima imegawanyika Nchi nzima kuongea na walimu kuhusu hilo lakini pia kutoa mrejesho wa mambo mbalimbali ambayo yanaendelea kutekelezwa na Serikali ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ili kurudisha hadhi ya mwalimu. Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema tuwambie anawapenda sana’’ amesema Mwalimu Nussu

Aidha, Mwalimu Nussu amewathibitishia walimu wa wilaya ya Chunya kwamba kuanzia Mwezi Januari walimu wameendelea kulipwa madai yao huku akisema zaidi ya walimu 100 (104 walimu kutoka idara ya Elimu ya awali na Msingi, walimu 15 kutoka Idara ya Elimu Sekondari) watapandishwa madaraja kwa mseleleko kwenda Daraja wanalostahili baada ya takwimu kuonesha wanalipwa mishara ambayo sio ya daraja analostahili kuwepo

Naye Afisa kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Mwalimu Liliani Nyinge amewakumbusha walimu waliohudhuria kikao hicho kwamba wanapotekeleza majukumu yao wakumbuke kuzingatia uwezo wa mtoto mmoja mmoja kwanza, utayari wa mtoto huyo kujifunza, umri wake, pamoja na mazingira anayotoka. Mambo hayo manne kwa pamoja yakizingatiwa yanaweza kusaidia kuamua njia sahihi ya kuwasaidia wanafunzi hao na wakapata matokeo sahihi hatimaye kuwa msaada kwa familia zao hapo baadaye.

Awali akitoa taarifa ya Elimu katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya, Afisa Elimu awali na Msingi Mwalimu Ferd Y. Mhanze amesema, Halmashauri ya wilaya ya Chunya imenufaika sana na Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwakuipangia walimu wengi wilaya hiyo, tofauti na utaratibu wa kupanga watumishi uliokuwa unatumiwa hapo awali, Hivyo ameomba matumizi ya mfumo huo maalumu  wa kuwapangia walimu vituo vya kazi uendelee ili Wilaya ya Chunya iendelee kunufaika zaidi na hatimaye lengo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuwahudumia wananchi wake kwa kuwapatia Elimu bora litimie Chunya.

“Tunawashukuru TAMISEMI kwa kutumia mfumo maalumu kugawa walimu, kwani wilaya ya Chunya tumepata walimu wengi tofauti na ilivyokuwa hapo awali hivyo ni maombi yetu matumizi ya Mfumo huo wa kuwapanga walimu uendelee ili wilaya ya Chunya tuendelee kupata walimu wengi zaidi na kwakuwa tunashukuru na kushukuru ni namna nyingine ya kuomba hivyo tunaomba muendelee kuitazama Chunya kama mnavyoitazama sasa” Amesema Mwalimu Mhanze

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalimu Hamis M. Mapato kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wilaya ya Chunya amesema Halmashauri ya wilaya ya Chunya inafanikiwa kutekeleza vigezo vyote vya upimaji kutokana na ushirikiano mzuri pamoja na uwajibikaji wa walimu kutoka idara zote za Elimu Msingi na Sekondari.

“Mafanikio yaliyosomwa hapa katika taarifa ya Idara za Elimu ya awali na Msingi na Taarifa ya Idara ya Elimu Sekondari yamechagizwa na walimu hawa walioko mbele yako, Tumepita kwenye vituo vyao kuwahimiza kulingana na Vigezo vya upimaji wa ufaulu (Key Perfomrmance indicators KPI). Ndugu washiriki wa kikao hiki tunao ugeni wa Kitaifa umekuja kushuhudia namna tulivyo tekeleza vigezo vya KPI naomba kuwasihi na kuwaomba tusikilize na tumfuatile ili tupate lengo la Serikali kwetu” Amesema Mwalim Mapoto.

Kikao hicho kimehusisha walimu zaidi ya mia tatu na hamsini kutoka idara ya elimu ya awali na msingi, pamoja na idara ya elimu ya Sekondari wilaya ya Chunya, walimu wakuu, wakuu wa shule maafisa Elimu kata na watumishi wa idara za Elimu awali na msingi, idara za elimu sekondari, Idara ya Utumishi, Tume ya utumishi wa walimu (TSC) Ofisi ya Mdhibiti ubora sambamba na ugeni kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI

Afisa Elimu Sekondari na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalim Hamis M Mapoto akizungumza wakati wa kikao cha walimu mbele ya viongozi kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI mapema leo kwenye ukumbi wa Mikutano Sapanjo

Afisa Elimu awali na Msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya akiwasilisha Taarifa ya Elimu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mbele ya walimu na wagenzi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI leo katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Baadhi ya walimu kutoka Idara ya elimu awali na msingi pamoja na walimu kutoka Idara ya Elimu Sekondari ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakisikiza kwa makini maelekezo na Mafunzo kutoka Viongozi Ofisi ya Rais TAMISEMI mapema leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo)

Mkurugenzi msaidizi Elimu anayesimamia elimu ya awali na Msingi Kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mwalimu Suzana Nussu akiendelea kuwasilisha namna ambavyo Serikali ya awamu ya sita inatekeleza mambo mbalimbali ili kurudisha hadhi na heshima ya Mwalimu nchini

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.