• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Milioni 50 kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya Ifumbo

Imewekwa: June 18th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Mbeya Mh. Juma Z. Homera ameagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuhakikisha wanapeleka fedha kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya Ifumbo ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi.

Homera ametoa maagizo hayo aliposhiriki katika kikao maalam cha Baraza la Hoja ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ina jumla ya hoja 17 ambazo hazijapatiwa majibu.

“Tafuteni milioni 50 pelekeni pale na kama hamjatenga kwenye bajeti tafuteni hela ziende na sisi tunachotaka katika moja ya hoja zitakazojifunga kwa mwaka ujao wa fedha na hiyo hoja ya kituo cha afya Ifumbo kiwe kimeshakamilika” amesema Homera

Homera ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kufanya uhamishaji wa fedha ili kuweza kuhakikisha wanapeleka hela kwenye kituo hicho.

“Fanyeni reallocation {uhamishaji} pelekeni milioni 50 kwenye hicho kituo hayo ni maelekezo nikifika tena hapa nikakuta hamjapeleka hatutaelewana,” alisema Homera.

Homera aliongeza kusema kuwa, wananchi wa Kata ya Ifimbo wanapata sana shida kufuta huduma za afya wanatembea zaidi ya kilometa 35 kupata huduma za afya katika hospitali ya wilaya.

“Mama na mtoto wanapoteza maisha yao kwa kushindwa kufika katika Hospitali ya Wilaya, wanafia njiani na sisi tumo humu ndani Madiwani, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na wataalam tunashindwa kutafuta milioni 50”

Pia Homera aliongeza kwa kusema kwa kuwa wananchi wa Kata ya Ifumbo wanapata shida, hakuna haja ya kuchelewa, Halmashauri itafute fedha na kupeleka ili kukamilisha ujenzi wa hicho kituo.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Homera ameutaka uongozi wa Halmashauri kuhakikisha wanawashirikisha waheshimiwa madiwani katika miradi yote inayotekelezwa na wafahamishwe kiasi cha fedha kinachotolewa.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Ifumbo, Mh. Weston Mpilya amesema ujenzi wa kituo cha afya Ifumbo ulianza tangu mwaka 2016 na mpaka sasa bado hakijakamilika kitu ambacho kinasababisha wananchi kupata adha ya huduma za afya.

“Jiografia ya eneo letu mpaka tunaifikia Hospitali ya Wilaya ni umbali mrefu sana na miundombinu ya barabara sio mizuri na kusababisha watu kupoteza maisha wakifuata huduma za afya,” alisema Mpilya.

Hamlashauri ya wilaya ya Chunya katika mwaka 2020/2021 ilitekeleza shuguli mbalimbali kwa ajili ya kuwaletea wananchi wake maendeleo

Shughuli zilizofanyika zililenga kuimarisha ustawi wa wananchi wa chunya ili wajiletee maendeleo, shughuli zote zilifanyika kwa kuzingatia miongozo mbalimbali ya serikali katika kuhakikisha matumizi ya rasilimali watu, fedha na rasilimali zilizopo katika halmashauri zinatumika kwa kuzingatia sheria.

Katika ukaguzi wa matumizi ya fedha na rasilimali kwa mwaka wa 2020/2021, halmashauri ya wilaya ya chunya imepata Hati inayoridhisha, Kwa mwaka huo halmashauri ilikuwa na hoja 47 ambapo zilikuwa zimetolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, hoja thelathini {30} zimefungwa na hoja Kumi na Saba {17} zinaendelea kutekelezwa

Aidha halmashauri ilikuwa na maagizo Saba {7} ya kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, maagizo matatu {3} yametekelezwa na maagizo manne bado yanaendelea kutekelezwa.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mh Mayeka S. Mayeka Akizungumza kwenye kikao maalumu cha Baraza la Hoja

Wahshimiwa Madiwani kutoka kata mbalimbali za halmashauri ya wilaya ya chunya wakiwa kwenye kikao maalumu cha Baraza la Hoja za Mkaguzi wa Hesabu za Halmashauri

Wakuu wa Idara na Vitengo mbalimbali wakifuatilia kwa makini kikao maalumu cha Baraza la Hoja

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mh. Bosco Mwanginde ambaye ni Diwani wa kata ya Mbugani akiwasilisha hoja kwenye kikao maalumu cha Baraza la Hoja 

Kaimu Mkurugenzi Ndg Curthbert Mwinuka Akifafanua jambo kwenye Kikao maalumu cha Baraza la Hoja za Ukaguzi wa Hesabu za Halmashauri


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.