• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Mifuko 20 ya saruji yachangiwa kuboresha huduma ya mama na mtoto

Imewekwa: March 6th, 2022

MDAU wa Maendeleo Wilaya ya Chunya Bi. Veronica Masache amechangia mifuko 20 ya saruji katika ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya cha Lupa.

Bi. Veronica ambaye ni mke wa mbunge wa Jimbo la Lupa ametoa mchango huo Machi 5, 2022 kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake yaliyofanyika kiwilaya kwenye Kata ya Lupa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Mimi kama mama katika zoezi zima mlilolianzisha la ujenzi wa wodi ya mama na mtoto kwenye kituo chetu cha afya cha Lupa niliwaahidi tutakuwa pamoja kwenye hili,” alisema Bi Veronica.

“Na kwa kuanza, leo naomba nikabidhi mifuko ishirini ya saruji, kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika kituo chetu cha afya hapa Lupa, huu ni mwanzo, tutaendelea kujitoa na tuendelee kuonesha jitihada kwa sababu hili linafanyika kwa ajili yetu sote.” Alisisitiza Bi Veronica.

Wanawake wa jamii ya Lupa kufuatia changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wakati wanakwenda kupata huduma za afya kwenye kituo cha afya, zimewapelekea kuanzisha mchakato wa ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili kutatua kero wanazokumbana nazo.

Kwa upande mwingine Bi. Veronica amewasisitiza wanawake na wote walioshiriki katika maadhimisho hayo kujitokeza kuhesabiwa wakati wa zoezi la sensa litakapowadia.

“Mwaka huu ni mwaka wa sensa, itakapofika kipindi cha sensa tujitokeze tuhesabiwe, maendeleo yana nyanja nyingi sana, ikijulikana idadi ya kaya zetu na watu ni moja ya kuleta maendeleo katika jamii zetu hivyo tulizingatie hilo.” Alisema Bi Veronica.

Aidha amewataka wanawake wahakikishe wanaitumia fursa iliyotolewa na Mh. Rais Samia Suluhu Hassan ya wanafunzi wa kike waliopoteza nafasi ya kusoma kuwarejesha mashuleni ili wakapate elimu.

Akisoma risala ya wanawake Kata ya Lupa, Bi. Dorice Paul Boma, alitaja baadhi ya changamoto ambazo wanakabiliana nazo kuwa ni uhaba wa watoa huduma za afya katika kituo cha afya pamoja na ukosefu wa nyumba za watumishi.

“Sisi wanawake wa Lupatingatinga kwa pamoja tumetambua na kuona changamoto kubwa tunazokumbana nazo katika kituo chetu cha afya zinatuathiri moja kwa moja, hivyo tukaazimia kuanzisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto, eneo hili sio muhimu tu kwa jamii ya wanalupa bali pia litasaidia jamii za jirani hasa katika kuhakikisha usalama wa mama na mtoto kabla na baada ya kujifungua.” Alisema Bi Dorice.

Aidha, kaulimbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani inasema, "Kizazi cha Haki na usawa kwa Maendeleo Endelevu, Tujitokeze Kuhesabiwa", ambapo maadhimisho hayo huadhimishwa kila mwaka Machi 8.

Bi Veronica Masache Akikabidhi Risiti ya Manunuzi ya Saruji kwa Mwenyekiti wa Kamati katika Maadhimisho wa Siku ya Wanawake wilaya ya Chunya yaliyofanyika Katika kata ya Lupa

Afisa Maendeleo ya Jamii halmashauri ya wilaya ya Chunya Bw. James Sunge akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri katika Maadhimisho ya siku ya wanawake ambapo kiwilaya yalifanyika kata ya Lupa

Umati wa Wananchi waliojitokeza katika Maadhiisho ya siku wa Wanawake Kiwilaya kata ya Lupa halmashauri ya wilaya ya Chunya

Katibu wa Maandalizi ya Serehe ya kilele cha Siku ya Mwanamke Bi Dorice Boma  Akiwasilisha risala ya Wanawake wa Jamii ya Lupa kwa Mgeni rasmi maadhimisho hayo kiwilaya yamefanyika Kata ya Lupa Halmashauri ya wilaya ya Chunya


Vijana wakike wakionyesha Umahiri wao wakuruka sarakasi  kwenye madhimisho ya siku ya wanawake  wilaya ya Chunya katika kata ya Lupa

Wanawake wakiwa kwenye Maadhimisho ya Siku yao Kiwilaya imefanyika kata ya Lupa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.