• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KERO YA MAJI KIJIJI CHA ITUMBI YAPATIWA SULUHU

Imewekwa: February 12th, 2023

Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Juma Aweso amesema ndani ya wiki MOJA milioni miatano italetwa mbeya ili kutatua changamoto ya maji katika kijiji cha Itumbi na Mwala ikiwa ni kuendelaza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2020-2025, ifikapo 2025 wananchi waishio vijijini wapate maji kwa asilimia themanini na tano (85%) tofauti na ilivyosasa ambapo wananchi vijijini wanapata maji kwa asilimia sitini na tatu (63)

Mhe: Aweso amesema hayo jana tarehe 11/2/2023 katika hafla ya utiliaji saini mkataba wa ujenzi mradi wa maji kutoka mto Kiwira iliyofanyika Jijini Mbeya katika viwanja vya shule ya Msingi Hasanga Mkabala na mizani uyole, Mradi ambao unataraji kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 117 ambapo maji lita milioni 180 zitazalishwa kwa siku wakati mahitaji kwa sasa ni lita milioni tisini (90)

“Nimepata maombi kutoka kwa mkuu wa Mkoa, nimepenyezewa maombi na spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia nimepata maombi kutoka kwa Naibu waziri wa Maji kwamba kuna changamoto kubwa ya Maji Itumbi, Mheshimiwa Naibu waziri wa Maji tukitoka hapa tukafanya mawasiliano na katibu mkuu wizara ya maji ili ndani ya wiki moja, shilingi milioni mitano (500) zije mbeya kutatua kero ya Maji katika kijiji cha Itumbi na Mwala”

Aidha Mhe Aweso amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu hassan amesema niwaambie kwamba ahadi zote alizowaahidi wanambeya atazitekeleza na amesema anawapenda sana wana mbeya na anawaamini sana.

Maelezo mahususi aliyonipatia kwa wana mbeya ni haya; Rais ameniagiza niwambie wana Mbeya kwamba ahadi zote alizoziahidi kwa wana Mbeya atazitekeleza”

Sambamba na hilo Mhe Aweso amsema Rais Samia na serikali anayoiongoza imeadhimia kumtua ndoo Mama kichwa hivyo imenunua gari (mtambo) la kuchimbia visima vya maji kwa mikoa yote ya Tanzania na amemwagiza Naibu waziri wa Maji na Umwagiliaji kuhakikisha anakabidhi gari hiyo kwa Mkuu wa Mkoa ili eneo ambalo kuna shidaa ya Maji basi kuchimbwe visima ili wananchi wasihangaike kupata Maji

“Mhe Spika naomba nikupe salamu za wizara ya Maji na maelekezo ya Mhe Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Nchi yetu katika mikoa yote 25 serikali imenunua mitamboi maalumu ya kuchimbia visima vya maji kwa maeneo ambako wananchi hawana maji. Nakuagiza Naibu waziri Kabla haujaondoka Mbeya Wiki hii uwe umekabidhi gari ya kuchimba visima kwa Mkuu wa Mkoa”

Awali akizungumza Mbele ya waziri wa Maji na umwagiliaji, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe; JUMA ZUBERI HOMERA alimweleza waziri uwepo wa Changamoto ya maji katika Kijiji cha Itumbi kilichopo kata ya Matundasi huku ikieleza namna Itumbi inavyochangia katika ukusanyaji wa dhahabu wilayani chunya ambapo Zaidi ya kilogramu 100 hupatikana kwa mwezi kutoka itumbi lakini eneo hilo maji imekuwa tatizo kubwa

“Kuna tatizo moja pale Itumbi wilayani chunya, Pale Itumbi wanazlisha kilogramu 100 za dhahabu kwa mwezi wanaleta pale chunya lakini wanachangamoto kubwa ya Maji tungeomba mweshimiwa waziri tusaidie pale waweze kupata maji safi na salama ili wachenjue vizuri dhahabu zao waongeze uzalishaji ili walete dhahabu za kutosha kwenye soko la dhahabu tupate fedha zaidi tuendelee kujenga miradi ya maji. Pia kule Mwala iliyoko Mbeya vijijini kuna changamoto kubwa ya Maji. Mweshimiwa waziri ukituletea milioni miatano pale Itumbi na pale Mwala milioni 500 kazi inaisha mweshimwa Aweso”

Hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwepo Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe Juma Aweso(Mgeni rasmi) spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Mhe Dkt Tulia Ackson Mwansasu, Mhe Oran Njeza Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini na Mwenyekiti wa wabunge wote mkoa wa Mbeya na viongozi wengine wakati wilaya ya Chunya Ikiongozwa na Afisa Tarafa Tarafa ya kiwanja Erick F.Nyoni akimuwakilisha mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka Simon Mayeka akiambana na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu TAMIMU KAMBONA

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona akiwa kwenye Hafla ya Utiaji saini mkataba wa Ujenzi wa mradi wa maji kutoka mto Kiwira iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Hasanga Jijini Mbeya




Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.