• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA YAPIGA HODI MBEYA.

Imewekwa: February 23rd, 2025

Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria ndugu, Eliakim Maswi amefungua mafunzo ya siku moja kwa wataalamu wa Halmashauri za Mkoa wa Mbeya utekelezaji wa Kampeni ya msaada wa kisheria wa Mama Samia huku akiwataka wataalamu kwenda kutoa msaada wa kisheria bure bila malipo kwa wananchi wasio na uwezo wa kulipa gharama za wakili kutatua changamoto zao za kisheria zinazowakabili

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo leo Februari 23, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, ndugu Eliakim Maswi amesema Wizara imekamilisha kampeni ya msaada wa kisheria katika mikoa 17 nchini ambapo amewataka wataalamu kwenda kutoa msaada huo wa kisheria kwa wananchi wasio na uwezo wa kulipa gharama za wakili ili kutatua changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili wananchi.

“Nimeona Watumishi wa Chunya hapa, kwasababu wananchi wanaonewa sana kuna mwananchi mmoja kapokonywa ng’ombe zake 57, mbuzi, kuku na punda na dalali wa mahakama huku maamuzi ya mahakama ni kuchukua ngo’mbe 20 yule ni mtanzania na yupo kwenye nchi yake hatuwezi kukubali hali hii iendelee” amesema Eliakim Maswi.

Aidha, Katibu Mkuu Maswi ametoa rai kwa washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha wanaenda kuwasaidia wananchi kwa kiasi kikubwa kwenye msaada wa kisheria kutatua changamoto zinazowakabili ikiwemo migogoro ya ardhi pamoja na mirathi.

Akizungumza mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya utekelezaji wa kampeni ya Msaada wa kisheria wa Mama Samia,  Wakili Athumani Bamba, Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, amesema nimepokea maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria kuhusu mgogoro huo wa mkulima wa Chunya na dalali wa mahakama huku akiahidi kufuatilia kwa karibu na kutafuta suluhisho la haraka.

“Awali sikufahamu kuhusu mgogoro huo, ndio nimesikia hapa, sasa baada ya mafunzo haya ninaenda kufuatilia kwa karibu kujua suala hili kwa undani wake, nimpate huyo mkulima, nimpate dalali na nijue mahakama gani imetoa uamuzi ili tumsaidie huyu mkulima apate haki yake na ikiwezekana mifugo yake iweze kurudi” amesema wakili Bamba.

Akitoa mada kwa washiriki wa mafunzo ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia,Mkurugenzi wa huduma za kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Mwasheria Ester Msambazi amesema lipo ombwe kubwa la wananchi kutokuelewa sheria ndio maana Wizara ikaja na msaada huu wa kisheria ambayo inajulikana kama Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) ambapo malengo ya Kampeni ni kuongeza uelewa wa wananchi kutatua migogoro.

Wataalamu kutoka kwenye Halmashauri za mkoa wa Mbeya wamehudhuria mafunzo ya msaada wa kisheria wa Mama Samia ambapo wataalamu hao watatoa huduma ya msaada wa kisheria kwa muda wa siku kumi bila malipo kwa wananchi wa Halmashauri za Mkoa wa Mbeya.

Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria ndugu, Eliakim Maswi akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wakati wa uzinduzi wa Mafunzo ya kampeni ya msaada wa Kisheria wa Mama Samia uliofanyika leo Februari 23, 2025 katika ukumbi wa Mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Mtoa mada wakiwasilisha kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akiwasilisha andiko lake kwa washiriki wa mafunzo ya utekelezaji wa msaada wa kisheria wa Mama Samia kutoka katika Halmashauri za Mkoa wa Mbeya.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.