• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Kamati ya Siasa Mkoa kukagua miradi ya maendeleo Chunya

Imewekwa: March 19th, 2022

WAJUMBE wa Kamati ya Chama Cha Mapinduzi {CCM} Mkoani Mbeya na Wilaya ya Chunya wamefanya ziara ya siku mbili kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo Wilayani Chunya.

Kamati imetembelea miradi ya Idara ya Afya, Idara ya Elimu sekondari, Mradi wa Barabara chini ya TARURA na Mradi wa Maji unaotekelezwa na RUWASA.

Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoani hapa, Mhe. Mohamed Mashango ameonesha kuridhika na utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Akizungumza katika ziara hiyo Mhe. Mashango amesema, ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi hasa miradi ya Afya ambapo Halmashauri inatekeleza ujenzi wa kituo cha Afya Kambikatoto, Mafyeko pamoja na ujenzi wa wodi ya wanawake na wanaume, ujenzi wa Bohari ya Dawa na Jengo la Upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Chunya.

“Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya niwape hongera na kuwapongeza kwa muda mliopewa na hatua nzuri iliyofikia, na kama mlivyotoa ahadi ndani ya mwezi mtakuwa mmekamilisha basi hakikisheni mnakamilisha kama mlivyoahidi." Alisema Mashango.

“Tumeona kule kwenye ujenzi wa kituo cha afya majengo yamefika kwenye asilimia kubwa zaidi na kwa kasi ya ujenzi huu wa nyumba ya madaktari tumeridhika nayo." Aliongeza Mhe. Mashango.

Aidha, Mhe. Mashango alieleza matarajio yake katika ujenzi wa miradi hiyo,na kuwahimiza wajenzi kukamilisha kazi haraka iwezekanavyo ili wananchi waanze kupata huduma.

"Kwa hiyo matarajio yetu ni kwamba katika kipindi hicho ambacho mmeahidi, tukija kwa mara nyingine tutakuta matarajio makubwa zaidi, kwamba tutakuta angalau watu wameshaanza kupata huduma na huku tukute Madaktari wamekaa itakuwa nzuri zaidi ili kuwapunguzia watu adha wanayoipata." Alisema Mhe. Mashango.

Kwenye kituo cha Afya Kambikatoto kamati imeushauri uongozi wa Halmashauri kuchukua hatua za haraka za kuchimba kisima ili kuhaikisha kituo kinakuwa na maji pindi mchakato wa kupata maji ukiendelea.

“Ni vizuri pakawa na mpango wa kuchimba kisima kama ambavyo mmesema, maeneo haya maji ukiyatafiti yanapatikana, tumejifunza pale kijijini watu wamechimba visima wamepata maji, vizuri pakawa na kisima hata kimoja ili kusaidia kutoa huduma hapa.” Alisema Ndg Charles J Seleman Katibu wa CCM Wilaya ya Chunya.

Kwa upande wa mradi wa Eimu Sekondari kamati haikuridhika na kasi ya utekelezwaji wa mradi huo unaojengwa kwa nguvu za wananchi kwani unakwenda taratibu na umechukua miaka mingi bila ya kukamilika.

Kamati imeutaka uongozi wa Kata ya Mafyeko kwa kushirikiana na Halmashauri kuchukua jitihata za haraka kuhakikisha ujenzi wa sekondari ya Mafyeko unakamilika ili mwakani isajiliwe na watoto waanze kusoma, ili kuwapunguzia watoto adha ya kutembea umbali mrefu pindi wanapokwenda shuleni.

Kamati ya Siasa Mkoa kweye ziara hii waliambatana na Wataalamu wa Sekretarieti ya Mkoa, Wataalam wa Wakala wa Serikali TARURA, RUWASA pamoja na Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Chunya, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Chunya, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mh. Mayeka Simon Mayeka wakwanza kushoto akiwa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Mhe. Mohamed Mashango wa Katikati pamoja na Katibu wa CCM Wilaya ya Chunya Ndg Charles Seleman wakati wa Ziara ya Kamati ya siasa Mkoa na Wilaya kukagua utekelezaji wa Miradi ya maendeleo wilaya ya Chunya.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndg Tamim Kambona wa kwanza kulia akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Mh. Mohamed Mashango wakati wa ziara ya kamati ya Siasa Mkoa na wilaya walipotembelea wilaya ya chunya kukagua Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya wakikagua Ujenzi wa Sekondari ya Mafyeko wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo Wilayani Chunya.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa na Wilaya ikiongozwa na Mwenyekiti wa Vijana UVCCM mkoa wa Mbeya Mh. Mohamed Mashango wakikagua ujenzi wa wodi ya Wanawake na wanaume katika hospitali ya wilaya.

Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya wakikagua Ujenzi wa Kituo cha Afya Mafyeko wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo Wilaya Chunya.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.