• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

HAKUNA MALIPO YOYOTE YATAKAYOPITISHWA BILA KULIPA DENI RUWASA

Imewekwa: June 25th, 2024

Katibu tawala wa wilaya ya Chunya ndugu Anakleth Michombero amezitaka taasisi zote za Serikali zinazodaiwa na RUWASA wilayani Chunya kulipa mara moja madeni yao huku akisema hakuna malipo yoyote yatakayofanyika kwa taasisi zote ambazo ziko chini ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya mpaka watakapokuwa wamelipa madeni yao kwa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira RUWASA.

Akizungumza leo tarehe 25/05/2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati akimwakilisha Mkuu wa wilaya ya Chunya kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo vyomba vya utoaji maji (CBWSO) vilivyopo ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya lengo likiwa ni kuhakikisha vyombo hivyo vinajiendesha

“Naomba kutoa maelekezo ambayo Mkuu wa wilaya ameniagiza, Taasisi zote zenye madeni mfano Shule ya Msingi Mapogolo pamoja na Zahanati ya Mapogolo kuhakikisha wanalipa madeni yote, na hili tunaanza sasa hivi kulishughulikia maana taasisi hizo zote ziko chini ya Mkurugenzi hivyo hakuna malipo yoyote yatafanyika mpaka tuone taasisi hizo zimelipa madeni yao kwa RUWASA”. Amesema Michombero

Aidha amewataka viongozi wa Serikali na wadau wengine kutambua mipaka yao ya utendaji kazi jambo ambalo litasaidia kuepusha mwingiliano na migongano ya majukumu kwa viongozi wa Vyombo na viongozi wengine katika eneo husika na kwakufanya hivyo itasaidia vyombo hivyo kuongeza upana wa matumizi ya maji kwa wananchi wa maeneo husika

“Niwaombe sana kila mmoja atambue majukumu yake na wakati mwingine kuheshimu mamlaka moja haikufanyi wewe kuondolewa nafasi yako, Mfano mimi ni mjumbe kwenye kamati mbalimbali na nikiwa katika vikao hivyo natambua muda wa kuwa mjumbe na natambua muda wa kuwa DAS, Hivyo niwaombe viongozi wenzangu kila mmoja atambue mipaka ya majukumu yake” Ameongeza Michombero

Mwakilishi wa meneja wa RUWASA Mkoa wa Mbeya Mhandisi Erasto Vincent Saronga amesema mafanikio makubwa yaliyopo ndani ya RUWASA Chunya yanachagizwa na ushirikiano mzuri uliopo katika ya uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya na uongozi wa RUWASA Chunya, na ameomba ushirkiano huo uendelee ili kwa pamoja waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa

Naye kaimu meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga amesema lengo la RUWASA kuwajengea uwezo viongozi wa vyombo wa watumia maji ni kuhakikisha wanasimamia vizuri makusanyo ya fedha za maji kwenye miradi yao na kuwaongoza katika matumizi bora ya fedha hizo na hatimaye waweze kutatua changamoto za mradi wa maji kwa wakati na kwa uwazi ili wananchi waweze kupata taarifa zote kuhusu miradi ya maji iliyo katika maeneo yao wanayoishi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde amewataka washiriki wote kufuatilia vizuri maelekezo hayo huku akiwahakikishia Madiwani waliopo kwenye maeneo ya miradi ya maji yanayosimamiwa na wananchi kupitia vyombo vya watumia maji kwamba wanapowafuatilia kwa kuhoji maswali lengo lao ni kuona wananchi wanapata maji hivyo wakati mwingine wanaweza kuwauliza viongozi wa vyombo vya watumia maji ili kujiridhisha na mwenendno wa utoaji wa maji kwa wananhi wake.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ndugu Tamim Kambona amewataka viongozi wa watumia maji Chunya kuhakikisha wanasimamia vizuri makusanyo ya fedha ili kuweza kuhudumia miundombinu ya maji katika maeneo yao huku akiwataka kutochanganya fedha za maji na fedha nyingine za makusanyo yanayofanyika kwenye vijiji kwani Vyombo vya wasimamia maji ni taasisi inayojisimamia tofauti na taasisi nyingine katika vijiji

Mafunzo hayo yamefanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) yakihudhuriwa na Viongozi wa Vyombo kutoka kwenye maeneo husika, madiwani kutoka kwenye maeneo ya miradi husika, watendaji wa kata pamoja na maafisa wa RUWASA kutoka Mbeya na lengo likiwa ni kuwajengea uwezo viongozi hao katika kusimamia miradi ya maji iliyopo katika maeneo yao.

Mwakilishi wa meneja wa RUWASA Mkoa wa Mbeya Mhandisi Erasto Vincent Saronga akisema jambo mbele ya Katibu tawala wilaya ya Chunya wakati wa Mafunzo kwa wajumbe wa vyombo vya watumia maji wilaya ya Chunya

Kaimu meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga akionesha takwimu za Makusanyo ya Fedha za vyombo vya watumia maji kupitia mfumo (Huko anakoonesha ilikuwa ni eneo ambako projector ilitazamishwa na wataalamu ili kuonesha takwimu kwa mgeni rasmi)

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde akizungumza jambo wakati wa Kikao cha kuwajengea uwezo viongozi wa vyombo vya watumia maji wilaya ya Chunya mapema leo kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo)

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ndugu Tamim Kambona akizungumza kwenye kikao cha kuwajengea uwezo viongozi wa watumia maji wilaya ya Chunya kilichoketi mapema leo

Kaimu meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga akiwasilisha mada wakati wa Kikao cha kuwajengea uwezo viongozi wa vyombo vya watumia maji wilaya ya Chunya

Baadhi ya washiriki wa kikao cha viongozi wa vyombo wa watumia maji wilaya ya Chunya wakiendelea kufuatilia mafunzo na maelekezo kutoka kwa wawezeshaji wakati wa kikao kilichoketi leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo)

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.