• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

Imewekwa: May 14th, 2025

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewataka wakulima wa vyama vya ushirika wilaya ya Chunya kuhakikisha wanamiliki ardhi kwaajili ya matumizi ya sasa na hata matumizi ya baadaye ya vyama hivyo kwani ardhi inaongezeka thamani kila siku

Ametoa kauli hiyo mapema leo tarehe 14/05/2025 katika kijiji cha kalangali wakati akifungua rasmi kiwanda cha kusaga Unga na kukamua mafuta ya alizeti mali ya Chama Kikuu cha Ushirika cha wakuima wa Tumbaku Chunya (CHUTCU)

“Hata ninyi wenyewe mnaongoza wakulima ambao wana ardhi hivyo hata ninyi vyama vya ushirika hakikisheni mnamiliki ardhi na mkishakuwa na ardhi hakikisheni mnatafuta hati, hakuna kitu kinatafutwa kwasasa kama ardhi, jambo hili ni muhimu sana hapo mbeleni. Wekeni ardhi hiyo salama kwakuikatia hati ili kiongozi atakayekuja na anauchu na ardhi asiweze kuitafuna” amesema Batenga

Aidha Mhe Batenga amevitaka vyama vtote wananchama kuongeza juhudi ya kulima mahindi na Alizeti ili kuhakikisha kiwanda hicho kinapata malighafi za kutosha jambo ambalo kwanza linawatea wakulima faida kwakuwa soko la mahindi la uhakika lipo lakini faida itakayotokana na uzalishaji wa unga wa kutosha na kuuza huku akihimiza kuongeza juhudi ya kutafuta masoko ya bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.

“Vyama vya msingi wekeni utaratibu wa kuona namna ambavyo mtalisha kiwanda hiki ili malighafi ziwepo maana kiwanda kina uwezo wa kufanyakazi masaa ishirini na nne hivyo kwa kuwepo malighafi za kutosha kutasaidia kiwanda kuzalisha kwa kiwango stahiki na hatimaye mtapata faida zaidi” ameongeza Mhe Batenga.

Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Mbeya Bwana Richard Edlia amesema ufunguzi wa kiwanda hicho ni tafsiri ya moja kwa moja ya Maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani ya kuongeza thamani mazao ya wakulima kwani kiwanda hiki moja kwa moja kitaongeza thamani ya Mahindi na alizeti za wakulima wa wilaya ya Chunya.

Awali akitoa taarifa za ujenzi wa kiwanda hicho Bwana Fransisco Chidege amesema lengo la ujenzi wa kiwanda hicho ni kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima wa Mahindi na Alizeti wa wilaya ya Chunya kwa kupata eneo la kuuza mazao yao kwa bei nzuri jambo ambalo litaendelea kuwanufaisha na kuongeza uchumi wa mkulima mmoja mmoja na hatimaye uchumi wa Taifa kwa ujumla

Hafla ya ufunguzi rasmi wa kiwanda cha kusaga unga wa Mahindi na kukamua mafuta ya Alizeti  kilichogharimu shilingi milioni mia nne sitini na saba imefanyika leo ambapo Mkuu wa wilaya ya Chunya alikuwa mgeni rasmi. Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka vyama vyote vya msingi vilivyopo mkoa wa kitumbaku Chunya pamoja na wananchi wa karibu na eneo kilipo kiwanda hicho.

Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Mbeya Bwana Elia Richard akitoa neno wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi wa kiwanda

Bwana Fransisco Chidege (Mhasibu wa CHUTCU) akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kiwanda mbele ya Mgeni rasmi mapema leo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga (Kulia) akisikiliza Msomaji akisoma kibao kinachoonesha maandishi hapo ukutani naada ya kufungua rasmi kiwanda hicho

Unga unaozalishwa kwenye kiwanda kilichofunguliwa rasmi leo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.