• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YAJIPANGA KUENDELEA KUONGOZA MKOA WA MBEYA UKUSANYAJI WA MAPATO

Imewekwa: July 19th, 2024

Halmashauri ya wilaya ya Chunya kupitia kamati yake ya Mapamo kwa kushirikiana na wadau na wananchi wote wa wilaya ya Chunya inataraji kukusanya Shilingi Bilioni nane (8,747,616,000.00/=) kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 ambao umeanza mapema Julai Mosi 2024.s

Akitoa ufafanuzi wakati wa kikao cha Mapato kilichoketi leo katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ulipo kwenye jengo jipya la utawala Mwenyekiti wa kamati ya Mapato wilaya ya Chunya Adv. Athuman Bamba amesema ili kufikia malengo ni lazima Halmashauri ikusanye milioni 125 kila wiki lakini pia vikao vya kila wiki vitasaidia kufanya tathimini wa mwenendo wa ukusanyaji wa Mapato hayo ili kubadili utaratibu na kuongeza nguvu ya ufuatiliaji pale itakapotakiwa kufanya hivyo

Wajumbe wa kikao hicho wamekubaliana kwamba kila mmoja mwenye jukumu katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato kuhakikisha anatekeleza jukumu lake ipasavyo huku watendaji wa Kata wakitakiwa kuongeza juhudi katika maeneo yanayowahusu moja kwa moja.

Kupitia kikao hicho wajumbe wamepata wasaa wa kujadili kwa kina namna watakovyokusanya mapato katika vyanzo ambavyo vilikuwepo mwaka uliopita na vile ambavyo havikuwepo mwaka uliopita lakini mwaka huu vipo, Vyanzo ambavyo havikuwepo mwaka uliopita ila mwaka huu 2024/2025 vipo ni pamoja na Ada za Mabango,Kodi ya Majengo, Ushuu wa Maegesho ya Malori na Magari na Kodi ya pango la Ardhi.

Ikumbukwe mwaka wa fedha ulioisha hivi karibu 2023/2024 Halmashauri ya wilaya ya Chunya iliongoza Halmashauri za Mkoa wa Mbeya kwa kipindi chote katika ukusanyaji wa Mapato jambo ambalo liliwezekana kutokana na Juhudi ya Kamati ya Mapato, watendaji ngazi mbalimbali pamoja na ushiriki Mzuri wa wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Kupitia Mapato ya Ndani Halmashauri imeendelea kutekeleza miradi Mbalimbali ikiwepo Ujenzi wa Kituo cha Afya Sangambi, Ujenzi wa Shule ya Mchepuo wa Kingeleza, Ujenzi wa Soko la Madini na kwasasa Ujenzi unaoendelea ni ujenzi wa uwanja wa Michezo wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambapo pamoja na ushiriki mzuri wa wadau wa Maendeleo lakini pia Halmashauri ya wilaya ya Chunya nayo hushiriki kwa namna moja au nyingine katika kuchangia fedha lakini pia kuhakikisha Ujenzi huo unasimamiwa vyema na watalamu wake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mapato Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adv Bamba (Aliyenyoosha Mkono Mbele) akizungumza jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichoketi Mapema leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Jengo Jipya la utawala)

Afisa Biashara wa wilaya ya Chunya ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Mapato Ndugu Lodrick Mwakisole akizungmza jambo wakati wa Kikao cha Mapato mapema leo

Ndugu Paul Lugodisha ambaye ni afisa kilimo akichangia Jambo wakati wa kikao cha Mapato kilichoketi leo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.