• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TANGAZO KUTOKA KWA WAZIRI WA OR TAMISEMI

Imewekwa: November 10th, 2019

Zoezi la Uchukuaji fomu, Urudishaji fomu, Uteuzi, Pingamizi na Rufaa lilianza tarehe 29/10/2019 na kumalizika tarehe 9/11/2019.

Katika zoezi hilo jumla ya wananchi 555,036 kutoka Vyama mbalimbali vya Siasa walifanikiwa kuchukua fomu za kugombea. Na jumla ya wananchi 539,993 sawa na asilimia 97.3 walifanikiwa kurejesha fomu.

Wagombea kutoka Chama cha Mapinduzi waliochukua fomu walikuwa 412,872 (asilimia 74), Chama cha Demokrasia na Maendeleo walikuwa 105,937 (asilimia 19), Chama cha Wananchi CUF walikuwa 24,592 (asilimia 4), ACT Wazalendo walikuwa 8,526 (asilimia 1.5), NCCR – Mageuzi walikuwa 2,244 (asilimia 0.4) na Vyama vingine vyenye usajili

wa kudumu walichukua chini ya asilimia 0.1 kwa kila chama.

Katika zoezi zima la kuchukua na kurejesha fomu kulikuwa na changamoto kubwa kwa wagombea wengi kufanya makosa mengi ya kikanuni yaliyopelekea wengi wao kutoteuliwa. 

Baadhi ya makosa hayo ni pamoja na kujidhamini wenyewe, kutojaza fomu namba IV, kutofautiana kwa majina, kutojaza fomu kwa ukamilifu, kuandika umri, kukosea umri (mfano amezaliwa mwaka 2019) na makosa mengine mengi mbalimbali. Hii ilitokana na baadhi ya vyama kushindwa kuwajibika ipasavyo katika kuwaelekeza wanachama wao. Kutokana na hali hiyo pingamizi na rufaa mbalimbali zipatazo 15,380 ziliwasilishwa.

Hadi zoezi la maamuzi ya rufaa mbalimbali lilipohitimishwa tarehe 9/11/2019, jumla ya rufaa 4,921 (32%) zilipitishwa na zilizobaki zilikosa sifa kwa sababu mbalimbali.

 

Katika mchakato huo wa kuchukua na kurudisha fomu Chama cha Mapinduzi kimefanikiwa kupita bila kupingwa katika maeneo mbalimbali kwakuwa hapakuwa na mgombea yoyote kutoka Chama cha Upinzani. Kwa upande wa Wenyeviti wa Vijiji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vijiji 6,248 kati ya vijiji 12,319 sawa na asilimia 51. 


Kwa upande wa Mitaa Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika Mitaa 1,169 kati ya Mitaa 4,263 sawa na asilimia 27 Kwa upande wa Vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika Vitongoji 37,505 kati ya Vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58. Kwa upande wa Wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

 

Kwa kuwa imeonekana wazi wananchi kutoka vyama mbalimbali wamekuwa na nia kubwa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi licha ya vyama vyao kutokuweka umuhimu katika kuwaelekeza vyema wanachama wao juu ya ujazaji fomu kwa mujibu wa Kanuni. 


Mamlaka ya Uchaguzi imeona ni vyema wananchi hao kupewa nafasi ya kushiriki katika Uchaguzi kwani imejidhihirisha wazi hata baada ya vyama viwili vilivyojitoa bado wanachama wao waliendelea kuwasilisha rufaa zao ili wapewe nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.

 

Kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka 2019 Tangazo la Serikali Na. 371 la Mwaka 2019 Kanuni ya 49, Tangazo la Serikali Na. 372 la Mwaka 2019 Kanuni ya 51, Tangazo la Serikali Na. 373 la Mwaka 2019 Kanuni ya 52, na Tangazo la Serikali Na. 374 la Mwaka 2019 Kanuni ya 52 ninatoa muongozo kwamba Wagombea wote ambao walioteuliwa na kudhaminiwa na vyama vyao na kufanikiwa kurejesha fomu zao za uteuzi kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika kipindi kilichokuwa kimepangwa cha kuchukua na kurejesha fomu kilichoanza tarehe 29*/10/2019 na kumalizika tarehe 04/11/2019 kwa Tangazo hili wanapewa sifa ya kupigiwa kura na wananchi wa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika kwa ajili ya Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2019 isipokuwa tu kama atakuwa amekutwa na mambo yafuatayo:
 

1. Siyo Raia wa Tanzania,

2. Hajajiandikisha katika Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika,

3. Amejiandikisha mara mbili,

4. Amejidhamini Mwenyewe,

5. Hajadhaminiwa na chama chake cha Siasa,

6. Wamerejesha fomu watu zaidi ya mmoja kutoka chama kimoja kwa nafasi inayofanana ya Mwenyekiti wa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji kwa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika. Msimamizi Msaidizi hata wajumuisha wagombea hao katika orodha ya wanaopaswa kupigiwa kura,

7. Amejitoa kwa mujibu wa Kanuzi za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Tangazo la Serikali Na. 371 la Mwaka 2019 Kanuni ya 19, Tangazo la Serikali Na. 372 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20, Tangazo la Serikali Na. 373 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20, na Tangazo la Serikali Na. 374 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20.

 

Msimamizi wa Uchaguzi ataanza kupokea ratiba za kampeni kutoka katika Vyama vya Siasa kuanzia leo hii tarehe 10/11/2019 hadi kesho jioni kwa ajili ya kuziunganisha.

 

Tarehe ya matukio na shughuli zingine zote zinazohusu Uchaguzi huu zitaendelea kwa mujibu wa Kanuzi za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2019.

 

Selemani S. Jafo (Mb.)

WAZIRI WA NCHI – TAMISEMI

10 Novemba, 2019

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.