• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SERIKALI HAITAVUMILIA UHARIBIFU WA MAZINGIRA UNAOENDELEA WILAYANI CHUNYA

Imewekwa: April 5th, 2023

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe; BOSCO MWANGIDE amesema Serikali haitavumilia kuona uharibifu wa mazingira kwa sababu yoyote ile unaendelea kufanyika wilayani Chunya, Hivyo kila atakaye bainika kuharibu mazingira sheria, kanuni na taratibu zitazingatiwa ili kumuwajibisha mtu huyo

Mwanginde alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa kitongoji cha Idendeluka kilichopo kijiji cha Sangambi kata ya Sangambi na kueleza msimamo wa serikali kuhusu uharibifu wa mazingira unaofanywa kupitia Uchomaji wa Mkaa katika kitongoji hicho.

 “Wako watu ambao si waaminifu na wanaona miti hii kama ni zawadi yao peke yao, wanaanza kuifanyia fujo, wanaikata na kuwanufaisha wao peke yao kitu ambacho mimi kama mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Sitakubali kabisa kwani Mimi nipewa dhamana ya kusimamia shughuli za maendeleo Chunya hivyo katika kipindi change Mimi nitapambana nao sana hawa wanaoharibu Mazingira kwa manufaa yao”

Awali akitoa salamu kwa wananchi Diwani wa kata ya Chalangwa Mhe Haji Chapa amesema Mazingira hayana mipaka hivyo yeye kufika katika kata ya Sangambi ni kutambua umuhimu wa mazingira na hatimaye kushirikiana pamoja kuhakikisha mazingira yanatunzwa

“Uharibifu wa mazingira hauna mipaka kwani ukame hautasema miti imekatwa sana Idendeluka basi ukame utakuwa idendeluka, ukame utakuwa kote wilaya ya Chunya kwa ujumla, hivyo tumefika hapa ili tuweze kupambana kwa pamoja kuhakikisha tunalinda mazingira pamoja na uharibifu unaofanywa katika maeneo haya ni mkubwa sana”

Diwani mwenyeji wa Kata ya Sangambi Mhe JUNJULU NDETE amesema haiwezekani viongozi wetu wa kitaifa wanahangaika kupambana kuhakikisha mazingira yanalindwa lakini sisi tunaharibu mazingira bila utaratibu hilo halitavumiliwa kabisa

“Vyomba vya habari vinaeleza namna ambavyo makamu wa Rais Mhe Dkt Philip Mpango ameonekana maeneo mbalimbali akizindua program za kupanda miti maeneo mbalimbali je sisi ni akina nani tukate miti bila kupanda miti? Hili mimi sitavumila kabisa”

Innocent Lupembe afisa misitu Mkuu (TFS) wilaya ya Chunya amesema wilaya ya Chunya hasa katika kitongoji cha Idendeluka ina uharibifu mkubwa wa mazingira na ndio sababu kubwa iliyopelekea uwepo wa mkutano huo ili kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira ukizingatia eneo hilo mbali ya kuwa moja ya Chanzo cha Maji kuelekea bonde la usangu na hata maji kwaajili ya matumizi ya wananchi wanaoishi katika maeneo hayo

Mabadiliko ya tabia nchi yanasababishwa na uharibifu wa Mazingira hasa ukataji wa miti kwa ajili ya uchomaji mkaa na kilimo jambo ambalo linahitaji nguvu za pamoja kuhakikisha uharibifu huo unakomeshwa ili kuepukana na athari zinazoweza kujitokeza hapo Mbeleni ikiwepo ukame, njaa na hata mafuriko.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ataendelea na ziara hiyo ya kutoa elimu kuhusu Utunzaji wa mazingira na kueleza msimamo wa serikali juu ya utunzaji wa mazingira tena leo 5/4/2023 katika kijiji cha Shoga ambapo mkutano wa hadhara utafanyika katika Kitongoji cha Tukuyu, Lengo likiwa ni kuhakikisha mazingira yanakuwa salama kwa ustawi wa viumbe hai na jamii kwa ujumla.

Baadhi ya wazee na wananchi wa kitongoji cha Idendeluka wakimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya chunya Mhe. Bosco Mwanginde kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwa lengo la kutoa elimu juu ya Umuhimu wa utunzaji wa mazingira

Baadhi ya Viongozi wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kitongoji cha Idendeluka

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.