Madawati arobaini na moja (41) yaliyotengenezwa kwa ushirikiano wa Mama na mtoto wake yamekabidhiwa Shule ya Msingi Matwiga iliyopo kata ya Matwiga Halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa lengo la kusaidia wanafunzi katika zoezi la ujifunzaji na ufundishaji jambo ambalo litaleta hamasa ya kusoma bidii kwa wanafunzi wa Shule hiyo
Wakizungumza mapema leo tarehe 19/05/2025 wakati wakikabidhi wadawati hayo zoezi lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msngi Matwiga, mama na mwanaye wamesema maono ya kutoa madawati hayo yametokana na namna walivyoshirikishwa uhaba wa madawati shuleni hapo lakini moyo wa kutoka ulimo ndani yao ndiyo msukumo mkubwa wa kutengeneza madawati hayo
“Wazo la kutoa dawati hizi lilitoka kwa mwanangu na mimi niliamua kumuunga mkono kwa kutengeneza dawati 10 wakati yeye ametengeneza dawati 31 hivyo kufanya jumla ya madawati arobaini na moja. Niwaombe wakinamama wenzangu na hata vijana wengine kukumbuka kwao kwa kutumia mali au fedha ambazo Mungu amewapatia” Amesema Mhe Neema Mwakaniemba (Mama yake Lusajo)
“Kupata wazo ni jambo moja lakini kuchukua hatua ni jambo lingine, nilipopata wazo la kuleta dawati hapa shuleni nilimshirikisha Mama yangu lakini nilimhirikisha Mke wangu wote walinielewa ndipo nikaanza kutengeneza dawati hizi. Jambo kubwa nililolifikiri ni watu gani na wangapi nitawasaidia ndicho kilichonisukumu kufanya hivi, hivyo kijana Lusajo amesema kutaja gharama iliyotumika sio jambo muhimu kwangu” Amesmea Lusajo Mwakibibi
Diwani wa kata ya Matwiga Mhe Frank Malambughi amemshukuru Mhe Neema Mwakaniemba (Diwani viti maalumu Halmashauri ya wilaya ya Chunya kutokea kata ya Matwiga) pamoja na mwanaye kwa msaada wa madwati hayo huku akiwasisitiza wananchi wa Matwiga na hata wananchi wa Tanzania kwa ujumla kutumia tukio hilo kama Mfano bora na wa kuigwa
Naye Afisa Elimu kata ya Matwiga Mwalimu Monica Kulanga amesema tendo la kutoa madawati hayo kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Matwiga ni la Kiroho maana Malaika wa Mungu (Wanafunzi) wa kila hali wakiwepo yatima na wanafunzi mbalimbali watatumia kukalia wawapo darasa.
Mwalim Mkuu wa Shule ya Msingi Matwiga mwalimu Godfrey Kikoti ameshukuru sana wadau kutoa madawati hayo kwa Shule yake, akiongeza kuwa yatasaidia sana kupunguza wanafunzi kukaa wengi kwenye dawati moja jambo ambalo haliwavutii wanafunzi kupenda shule lakini uwepo wa madawati haya kutaongeza motisha kwa wanafunzi ya kusoma, motisha ya kufundisha kwa walimu pia itaongezeka
Madawati hayo yametolewa na Mhe Neema Mwakaniemba Diwani wa Viti maalumu Halmashauri ya wilaya ya Chunya pamoja na motto wake Ndugu Lusajo Mwakibibi na yamepokelwa na mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Matwiga huku Diwani wa Kata ya Matwiga Mhe Frank E. Malambughi na viongozi wengine wa Chama na Serikali wakishuhudia makabidhiano hayo
Baadhi ya Madawati yaliokabidhiwa leo katika Shule ya Msingi Matwiga iliyopo kata ya Matwiga Halmashauri ya wilaya ya Chunya
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali pamoja na wananchi wachache walioshuhudia zoezi la kukabidhi madawati mapema leo katika shule ya msingi Matwiga
Itigi Road
sanduku la posta: P.O box 73 Chunya
simu ya mezani: 025 2520121
simu ya mkononi: 025 2520121
Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz
Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.